Tuesday, June 1, 2010

Mwanamke huyo anayekisiwa kuwa na umri wa miaka 20 na ushee wa mji wa Zhuhai kwenye jimbo la Guangdong alienda hospitali akiwa hasikii chochote kupiti

Mwanamke huyo anayekisiwa kuwa na umri wa miaka 20 na ushee wa mji wa Zhuhai kwenye jimbo la Guangdong alienda hospitali akiwa hasikii chochote kupitia sikio lake la kushoto, yameripoti magazeti ya China.

Tukio hilo lilitokea baada ya mwanamke huyo kupeana mabusu ya nguvu ya kunyonyana ndimi na mpenzi wake kwa muda mrefu.

Baada ya tukio hilo, makala mbalimbali zimeandikwa kwenye magazeti ya China vijana wakionywa wapunguze tabia ya kunyonyana ndimi sana kuliko kawaida.

"Kunyonyana ndimi kwa kawaida hakuna madhara lakini watu inabidi wawe waangalifu kidogo", liliandika gazeti la China Daily.

"Wakati wa kunyonyana ndimi, presha toka kinywani huisukuma ngoma ya sikio nje na hivyo kusababisha sikio kupoteza usikivu wake" alisema daktari aliyemtibia msichana huyo alipokuwa akitoa maelezo sababu ya msichana huyo kuwa kiziwi sikio moja.

Maelezo zaidi kuhusiana na madhara ya mabusu ya kunyonyana ndimi yaliandikwa kwenye gazeti la Shanghai Daily, ambalo liliandika: "Busu la nguvu husababisha uwiano wa msukumo wa hewa ndani ya masikio kuharibika na hivyo kusabisha ngoma ya sikio kupasuka".

Madaktari wamesema kuwa mwanamke huyo aliyepoteza usikivu sikio moja ataweza kusikia tena kupitia sikio hilo baada ya miezi miwili.


Mtoto wa Miaka Miwili Anayevuta Sigara 40 Kwa Siku


Ardi Rizal mtoto mwenye umri wa miaka miwili ambaye amekuwa akivuta sigara 40 kwa siku amekuwa gumzo duniani baada ya video kutolewa ikumuonyesha mtoto huyo jinsi anavyovuta sigara kwa wingi huku akicheza na watoto wenzake.

Ardi alianza kuvuta sigara akiwa na umri wa miezi 18 lakini hivi sasa akiwa na umri wa miaka miwili wazazi wake wanalalamika kuwa amekuwa mvutaji sigara sugu kiasi cha kufanya vurugu kubwa sana anaponyimwa sigara.

"Ardi anaponyimwa sigara huwa mwenye hasira sana na hufanya vurugu na wakati mwingine hujibamiza kichwa chake ukutani", alisema mama yake Diana mwenye umri wa miaka 26.

Kutokana na unene wake na jinsi anavyovuta sigara kwa fujo, Ardi anashindwa kukimbizana na watoto wenzake.

Serikali ya Indonesia iliahidi kuipa familia ya Ardi zawadi ya gari jipya iwapo Ardi ataacha kuvuta sigara. Lakini jitihada zote za kumuachisha Ardi sigara zimegonga mwamba na badala yake Ardi huifanya familia yake itumie takribani Tsh. 8,000 kila siku kwaajili ya kumnunulia sigara.

Baba yake ambaye anafanya kazi ya kuuza samaki, haoni hatari inayomkabili mtoto wake na husema kwamba mtoto wake ana afya njema hana matatizo yoyote.

"Sina wasiwasi wowote kuhusiana na afya yake, Ardi ni mtoto mwenye afya njema", alisema baba yake kuwaambia waandishi wa habari.