Thursday, June 3, 2010

50 Cent Choka Mbaya, Ukimuona Huwezi Kumtambua

50 Cent alivyokuwa zamani kushoto na alivyo sasa kulia.(picha baadaye)50 Cent amejikondesha kwa kunywa maji na juice pekee ili aweze kuigiza kwenye filamu mpya ambayo jikoni ambayo inamuelezea nyota wa mpira wa miguu ambaye anaugua ugonjwa wa kansa.

50 Cent ambaye ana umri wa miaka 34 amekonda sana na amepungua uzito wake toka kilo 97 hadi kilo 72.

50 Cent amejikondesha ili kuleta uhalisia wa mgonjwa wa kansa katika filamu ya "Things Fall Apart", filamu hiyo 50 Cent ndiye nyota wa filamu na prodyuza msaidizi.

Wakati picha mpya za 50 Cent zilipowekwa kwenye mitandao jana watu wengi waligoma kuamini na kusema kwamba picha hizo ni uzushi tu wa kwenye mitandao.

Lakini 50 Cent ambaye jina lake halisi ni Curtis Jackson alijitokeza na kuthibitisha kuwa picha hizo ni za kweli.

50 Cent alisema kuwa baada ya kumaliza kuigiza kwenye filamu hiyo ataanza kula kama kawaida kurudisha mwili wake wa zamani.

No comments: